Kakaa/Dadaa…
Hivi unajua ni kwa nini kila siku unaamka umechoka hata kama ulilala masaa 8?
Kuna kitu kimoja tu kinakusumbua… akili yako haipumui.
Una mawazo mengi.
Stress.
Presha.
Mengine hata hujui yanatoka wapi.
Lakini yanakutesa.
Unasema huna muda.
Unasema maisha ni magumu.
Unasema nitapumzika nikiwa kaburini.
Lakini ukweli ni huu:
Ukikosa utulivu ndani yako…
Hakuna utakachofanikisha nje yako.
Sasa Tuseme Ukweli Wote….
Unajitesa Mwenyewe.
Umezoea kukimbizana na kila kitu.
Simu haikai mbali.
TV haizimwi.
Instagram haifungwi.
Magroup ya WhatsApp hayanyamazi.
Hali hii inakuua polepole.
Inakuondolea amani.
Inakurudisha nyuma.
Na mbaya zaidi…
Unadhani hiyo ndiyo kawaida ya maisha.
Achana Na Uongo Wa DUNIA.
Watu wengi hawajui siri hii…
Kuna njia moja rahisi sana ya kupata amani ya ndani.
Ya kutuliza kichwa.
Ya kujisikia safi hata ukiwa huna kitu.
Inaitwa tahajudi (meditation).
Dakika 10 tu kwa siku zinaweza kubadilisha kila kitu.
Watu wanasema…
“Ah hiyo ni ya Waasia.”
“Ni mambo ya yoga.”
“Ni mapepo.”
Lakini siyo kweli.
Tahajudi ni tiba ya kiroho, kiafya, na kisaikolojia.
Ni nafasi ya kuongea na nafsi yako.
Kusafisha akili yako.
Kusikiliza kilicho ndani yako..
Jifunze Kitu Hapa….
Meditation haichukui muda.
Haitaki pesa.
Haibagui dini wala elimu.
Unakaa tu kimya. Unavuta pumzi. Unawaza kwa utulivu.
Dakika 5. 10. 15.
Inatosha.
Kila siku.
Polepole, unajiona mtu tofauti.
Unaanza kuelewa maisha.
Unaanza kuishi kwa amani.
Ndiyo dawa ya wasiwasi.
Ndiyo suluhisho la stress.
Ndiyo siri ya watu wenye mafanikio makubwa.
Mimi Niliwahi KUPOROMOKA KISAIKOLOJIA.
Na nitakuambia ukweli huu…
Miaka michache iliyopita, maisha yalinigonga mkwara.
Nilikuwa nimechanganyikiwa.
Mara deni, mara pressure, mara msongo, mara mahusiano hayajakaa vizuri.
Siku moja nikakaa chini. Nikasema, Acha nijaribu hii tahajudi.
Nilikaa kimya. Nikavuta pumzi.
Nilianza polepole.
Siku ya kwanza… hakuna nilichosikia.
Siku ya pili… niliboreka.
Siku ya tatu… nililia.
Siku ya saba… nilitulia.
Na tangu siku hiyo…
Maisha yamebadilika.
Sina presha ya maisha.
Nimejifunza kujisikiliza.
Nimejifunza kuwa mtulivu hata dunia ikiwa inateketea.
Na leo, najisikia kuwa hai kwa mara ya kwanza.
Mwisho Wa SIKU…
Usubiri msiba ndipo uanze kujitafuta.
Usingojee maisha yakuchoshe kabisa ndio uanze kutafuta utulivu.
Anza leo.
Kaa chini.
Fumba macho.
Vuta pumzi.
Futa mawazo.
Sikiliza moyo wako.
Hapo ndipo utagundua kuwa utulivu hauuziwi upo ndani yako.
ELIMU UJUZI BLOG NI BLOG YA JAMII AMBAYO NDANI YAKE KUNA ELIMU , UJUZI , UBUNIFU , MAFUNZO MBALIMBALI , UTAALAMU , STADI ZA MAISHA. AKIBA . UWEKEZAJI , UJASIRIAMALI , DINI , SAIKOLOJIA , TEOLOJIA , FALSAFA , NIDHAMU , ELIMU YA PESA , KUSOMA RIWAYA / HADITHI , USHAIRI , MICHEZO YA KUIGIZA . KARIBU UPATE MAARIFA UWEZE KUJIAJIRI NA KUFANIKIWA KATIKA MAISHA.
Monday, May 12, 2025
MAKALA : UTULIVU , AMANI , FURAHA , UPENDO HAVIUZWI DUKANI VIPO NDANI YAKO , VIFUKUE UFURAHIE MAISHA---KUWA NA TAHAJUDI ( MEDITATION ) KILA SIKU KWA DAKIKA 5 .10 . 15 INATOSHA-------CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment